Philip Kaloki. [Photo/courtesy]Mwaniaji wa kiti cha ubunge eneo la kibwezi mashariki Philip Kaloki ametozwa faini ya shilingi laki tano kwa kukiuka kanuni za uchaguzi.Uamuzi huo umeafikiwa na kamati ya utekelezaji wa sheria za tume ya uchaguzi nchini IEBC , pale kaloki alipofika mbele yake kufuatia tuhuma za kuzua vurumai zilizoibuliwa dhidi yake na mbunge wa sasa Jesica Mbalu.Akitoa uamuzi huo mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati ameonya kuwa tume yake haitosita kumfungia nje Kaloki kwenye uchaguzi mkuu wa agosti, iwapo atakosa kulipa faini aliopewa chini ya masaa 24.

Do you have a lead on a newsworthy story? Share news tips with us here at Hivisasa!